CONTACT US:

CONTACT US:
Mobile : 0755 484866
EMAIL : socialworkertz@yahoo.com

Wednesday, April 15, 2009

JE NA HILI LINATAKA MUONGOZO WA MA AFISA USTAWI WA JAMII?

SOMA MAKALA HII YA KUSISI MUA YA BINTI ALIYE AMUA KUWAAMBUKIZA WENZIE UKIMWI. KISHA UTUTUMIE MAONI YAKO.

Ohio kilikuwa kiwanja kizuri ila tatizo ni kwamba kila anayepita pale anakujua halafu unatakiwa uonyeshe maungo yako hadharani. Mimi sikuzoea tabia hizo hivyo, nilivaa miwani yangu na kuacha mapaja nje tu waangalie wenyewe wakipenda watakuja.Kule Kwa macheni tatizo lake ni mashoga wengi sana. Yaani mwanaume anaweza akaja kutafuta malaya akakuchanganya wewe na shoga kwani mashoga wanaojiuza hawana tofauti na sisi wanawake tunaojiuza. Bilcanas nako kuzuri ila vitoto vidogo vingi, nilikuwa naogopa matatizo na vijana wa kule sikupenda kufanya mchezo na watoto hata kwa dau gani. Nilingoja wanaume wenye pesa zao tu.

Nikawa naenda Jolly Club kujiuza ili nipate fedha za kujikimu kimaisha. Pale nilikutana na kahaba mmoja mzoefu kwa jina anaitwa Aisha. Akaanza kunionyesha mambo kadhaa wa kadha kuhusu biashara ya ukahaba.Hapo ndio nilijufunza kwamba sio makahaba wote ni masikini au hawajiwezi. Kuna wengine pesa wanazo ila wanapenda kufanya ukahaba baada ya kuchoka na dunia, wengine walikuwa na wanaume wao wakaachika wakaamua kuja huku kwenda na mwanaume yeyote yule anayekuja.Wengine wana matatizo katika ndoa zao kama vile kupigwa na kadhalika wanaamua kuja huku kujiuza au kukaa huku ili kuepuka matatizo katika ndoa zao au uhusiano wao. Wengine ndio kama hivyo waume zao hawana nguvu za kutosha kufanya nao tendo la ndoa wanaamua kuwa makahaba kila mtu na lake na mambo yake pia.

Aidha, siku hizi wanaume wengi wanapenda kitu kinachoitwa JICHO (Watu wazima mtakuwa mmenielewa). Hii nayo ni soko kuu lakini mwanaume anaweza kuja kwako akihitaji huduma ya jicho na wewe hutoi, tayari utakuwa umekosa soko.Wengine wanakuja kukuchukua uende ukawahuhudumie kumbe lengo lao ni kukupiga picha za ngono wakati unafanya kitendo hicho haswa wazungu. Wengine wanakupa ufanye mapenzi na mbwa wao au wanyama wao wengine mambo yanaenda hivyo.Hata hivyo, biashara hii ya ukahaba ilinichanganyia sana kwa miaka 2 niliyoifanya na hakuna aliyenijua kama nina Ukimwi.

Siwezi kuhesabu ni watu wangapi nimefanya nao ngono lakini ni zaidi ya 300 siku zingine nafanya kazi na watu zaidi ya watatu kwa siku moja kwahiyo mambo yanaendelea halafu wengi hawakupenda kutumia mipira ya kiume yaani kondom walipenda kuja hivi hivi tu bila kinga.Na mimi nilikuwa nimeshaathirika nilichokuwa natafuta ni fedha za kuendeleza maisha yangu kwahiyo hata kama nikifanya ngono zembe bila kinga mimi hainiumi sana kwa kuwa nilishajua hali yangu sikuweza kuitengua sikuwa na chochote cha kufanya zaidi ya hiki.

Hii ilikuwa ni kulipiza kisasi kwa maasi ambayo yule kijana alinifanyia kuniambukiza UKIMWI kwa makusudi huku akijua kabisa ameathirika siku nyingi, kwakuwa aliamua kuniua basi na mimi naua wengi zaidi na sijali kuhusu dhambi hizi nilizozifanya na sijutii kabisa.Huku mitaani waliniita majina kama J-Lo wakati mwingine Salma Hayek yaani wale waigizaji maarufu duniani kwa urembo nilio nao. Hakuna hata mmoja aliyejua kuwa nimeathirika au la kwasababu yule kijana niliyekuwa naye kama mpenzi alikufa kifo cha ghafla watu walisema amekufa kwa presha.

Mitaani napo nilikamua kinoma, waume za watu walikuja mpaka mlangoni kwangu na magari yao, wananipakia na kunipeleka katika kumbi za starehe na sehemu nyingine nyingi sana wengine walinihonga mali na mambo kibao kisa wamenipenda wanataka ngono.Na kwa uhakika hawa wanaume niliwapanga nitakavyo na hakuna aliyeweza kutambua mimi nina wanaume wangapi na wanaishi wapi wengi walijua ni washirika wangu katika kazi zangu na mambo yangu mengine, kwanza sikupenda kuongea na mwanaume yeyote chumbani kwangu wote nilikuwa nawaambia tukutane mbali kidogo na nyumbani hasa katikati ya jiji.

ITAENDELEA...

No comments:

Post a Comment