CONTACT US:

CONTACT US:
Mobile : 0755 484866
EMAIL : socialworkertz@yahoo.com

Wednesday, December 16, 2015

SABABU ZA WATOTO KUHITAJI MALEZI YA BABA

Ndugu zangu

Watoto huhitaji malezi ya pande zote mbili bila kujali wazazi wao wako pamoja au la.
Wanaume wengi wamekuwa wakisahau hili nakuhisi mama ndie mwenye jukumu pekee la kulea watoto. Mara kadhaa hurudi usiku na kukuta watoto wamelala na hutoka asubuhi sana kabla hawajaamka pengine bila hata kujua wameamka vipi.

Zifuatazo ni sababu kadhaa kwa nini wazazi wanahitaji malezi ya baba:

KUMJUA MWANAUME
Utashangaa lakini sehemu ya kwanza ya mtoto kujua mwanaume ni mtu gani, anaonekana vipi na tabia zake ni kupitia baba. Unavyoishi na familia yako ndio hivyo mtoto atajua wanaume wote wako hivyo!

KUCHEZANAE
Akina baba hucheza kwa namna tofauti kidogo na watu wengine, mara kadhaa utasikia mama akigombana na baba pengine tu baba anatumia nguvu nyingi akiwa anacheza na mtoto akihisi atamuumiza! Akina baba hucheza kwa nguvu zaidi na hucheza na mtoto kwa muda mrefu zaidi hii humfanya mtoto ajihisi salama na mwenye furaha.

3. KWA AJILI YA TABIA
Utafiti unaonyesha kuwa watoto wanaolelewa na baba huwa na tabia bora zaidi kuliko watoto wanaolelewa na mama pekee.

MTETEZI WAO
Hakuna kitu mtoto huhitaji akiwa mdogo kama rafiki wa karibu. Watoto wadogo hasa wa kike hupenda sana kuwa karibu na baba yao, kwan huhisi salama zaidi akiwa na baba nan i mtu atakayemtetea kwa mama.

KUJIAMINI
Uwepo wa baba katika maisha ya mtoto humfanya ajenge hali ya kujiamini kwani huhisi siku zote kuna mtu nyuma yake kwa ajili ya kumtetea.

KUWA NA MAHUSIANO BORA
Zile tabia njema anazoziona kwa baba na mama ndio hivyo hivyo atafanya kwa mpenzi wake. Wazazi husahau kuwa Watoto hujiskia vizuri sana wanapoona hali ya mawasiliano mazuri kati ya wazazi wao hata wanapokua wametengana.

KUCHAGUA NJIA SAHIHI
Mtoto anaelelewa na mama tu huwa na njia moja tu! Nayo ni ya mama, ni vema mtoto kupata upendo wa wazazi wote wawili ili ajue ni njia ipi sahihi kwake.

MAWASILIANO
SIMU: 0686 484866
EMAIL: socialworkertz@yahoo.com

1 comment:

  1. Safi sana somo nimeliewa barabara, kumbe ndo maana najiamin ila dingi alikuwa mtata! kwa kipigo chenyew nilikipata haswa.

    ReplyDelete